Foreign Exchange Rates

DStv Advert_010224

DStv Advert_010224

SBT Tanzania Advert_291123

Monday 25 September 2017

AIRTEL YATOA PUNGUZO YA BEI KWA BIDHAA ZAKE

Meneja wa huduma kwa wateja Bi. Celine Njuju akionesha simu na vifaa vilivyopunguzwa bei katika maduka yote ya Airtel nchini, kulia ni Meneja mauzo wa bidhaa za mawasiliano Airtel Bw. Pascal Maziku. Ofa ya simu na vifaa hivyo vya mawasiliano pia inaambatana na ofa ya dakika za muda wa maongezi pamoja, bando la intaneti na SMS bila kikomo kwa meiji sita.

Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel Tanzania imetoa rai kwa wateja kuhakikisha wananunua bidhaa bora zinazopatikana kwenye maduka yake kwani imetoa punguzo kubwa ya bei kwa bidhaa hizo.

Haya yamesemwa na Meneja wa Huduma kwa wateja Celina Njuju huku akithibitisha kuwa bidhaa hizo zitakuwa zikipatikana kwenye maduka yote ya Airtel na hivyo kuwashauri wateja kuhahakisha kuwa wanatumia nafasi hiyo kujipatia bidhaa bora kwa punguzo la bei.

Tunataka wateja wafaidi fedha zao, siku zimepita ambapo Watanzania walikuwa wanaenda madukani na kununua bidhaa feki kwani kwa sasa tunazo bidhaa halisi kabisa ambazo zinapatikana kwa bei nafuu, alisema Njuju.

Kulingana na Njuju, Wingle USB Modem ambayo hapo awali ilikuwa ikipatikana kwa Tshs60,000 kwa sasa itakuwa ikipatikana kwa Tshs45,000 pamoja na kifurushi cha intaneti cha bure cha 5GB. Uzuri wa hii modem ni kwamba unaweza ukatumiwa na watu mpaka kumi kwa wakati mmoja, alisema Njuju huku akiongeza ya kwamba modem hii inafaa sana kwa watu wanaofanya kazi maofisini, wafanya biashara na wanafunzi.

Kampuni ya Airtel Tanzania pia imetoa punguzo la bei kwa Magnus Bravo Z11 ambapo hapo awali ilikuwa inauzwa Tshs79,000 lakini kwa sasa ni Tshs69,000 ambapo pia itakuwa na kifurushi cha bure cha 12GB, dakika 300 kupiga mitandao yote na sms 300 kwa muda wa miezi sita. Pia kwenye punguzo ni simu ya Huawei Y3C ambapo hapo awali ilikuwa ikipatikana kwa Tshs140,000 na kwa sasa itakuwa inauzwa Tshs100,000 na itakuwa na kifurushi cha 12GB, dakika 300 kupiga mitandao yote na sms 300 kwa muda wa miezi sita.

Wateja pia watajipatia simu aina ya FERO 280 kwa Tshs30,000 kutoka bei ya awali ya Tshs38,000 ambapo itakuja na 150MB, dakika 150 kupiga Airtel kwenda Airtel na sms 150 kwa muda wa miezi mitatu.

‘Natoa wito kwa wateja wa Airtel kujitokeza na kufaidika na punguzo la bei ya bidhaa hizi kwenye maduka yote ya Airtel nchi nzima kwani muda wa punguzo ni mdogo, alisema Njuju.

No comments:

Post a Comment