Foreign Exchange Rates

DStv Advert_020324

DStv Advert_020324

SBT Tanzania Advert_291123

Wednesday 8 March 2017

VODACOM TANZANIA KUANZA RASMI KUUZA HISA ZAKE KWA WAWEKEZAJI

Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Vodacom Tanzania, Ian Ferrao

Kampuni ya simu za mkononi nchini Vodacom Tanzania itakuwa kampuni ya kwanza inayotoa huduma za mawasiliano kuuza hisa zake katika soko la hisa la Dar es Salaam maarufu kama “DSE”. 

Hii inafuatia rasimu ya waraka wa matarajio (Prospectus) na maombi yaliyotumwa kwenye Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA) kukubaliwa.  CMSA ndiyo mamlaka inayosimamia masoko ya mitaji na dhamana nchini.
Uuzaji wa hisa za awali wa Vodacom Tanzania Limited PLC ni katika utekelezaji wa Sheria ya Posta na Mawasiliano iliyofanyiwa marekebisho na sheria ya Fedha mwaka 2016 ambayo inaagiza kampuni zote za simu za mikononi kuuza 25% ya hisa zao kwa umma.
Hisa za kampuni hiyo inayoongoza kwa kuwa na wateja wengi zaidi nchini, huenda sasa zikaanza kuuzwa muda wowote kuanzia wiki hii au wiki ijayo. 

Vodacom Tanzania inatarajia kuorodhesha asilimia 25 ya hisa zake katika soko la mitaji ambayo ni sawa ni hisa milioni 560 zitakazokuwa na thamani ya shilingi bilioni 476 huku kila hisa ikiuzwa kwa Tsh 850. 

 Hii ni hatua kubwa sana kwa Vodacom Tanzania ikizingatiwa kwamba kampuni nyingine za simu zinasuasua. Vodacom inatarajiwa kuwa miongoni mwa kampuni zitakazokuwa na mitaji mikubwa katika soko la DSE. 

Kampuni nyingine zenye mitaji mikubwa ni Acacia, EABL na TBL. Hadi hivi sasa DSE ina kampuni 25 zilizoorodheshwa ambapo kampuni za ndani ni 18 na zile zilizoorodheshwa kutoka masoko ya kigeni yakiwemo London na Nairobi ni 7.
Taarifa rasmi za mauzo ya awali ya hisa hizo milioni 560 lini zitaanza kuuzwa, na wawekezaji gani watakidhi vigezo zitatangazwa hivi karibuni. Tutazidi kukuletea taarifa hizi za uwekezaji kwa makampuni ya simu nchini.

No comments:

Post a Comment